Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 15:56

Serikali ya Tanzania Yazidi Kulaumiwa


Serikali ya Tanzania inaendelea kulaumiwa kwa kushindwa kutekeleza ulipaji wote wa malimbikizo ya waliokuwa wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika mashariki iliyovunjika mwaka 1977.

Kwa mujibu wa mwanasheria, Sengodo Mvungi aliiyepo katika mji mkuu wa nchi hiyo Dar es Salaam, hatua ya serikali kuwapiga marufuku wastaafu waliokuwa wakidai haki zao siyo sahihi na ni ukiukwaji wa haki za binadamu.

Bwana Mvungi amesema hakuna kipengele kinacho mkatalia mtu yeyote kudai haki yake kwa njia halali, na amewasihi wazee wastaafu wa jumuiya ya Afrika mashariki kuendelea na taratibu za kudai mabilioni ya fedha wanazoidai serikali.

XS
SM
MD
LG