Waziri wa mambo ya nchi za njee wa Tanzania Bw Bernard Membe amesema Tanzania, kama mwenyekiti wa AU inapinga hatua ya mwendesha mashtaka wa mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa vita kumfungulia mashtaka Rais Omar al-Bashir, kwa ajili ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu. Mwandishi wetu wa Dar es Salaam Dinah Chahali anaripoti.