Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 18:49

Afisa wa chama cha CHADEMA Saanane hajulikani aliko


Ben Saanane msahuri wa mweneyekiti wa CHADEMA
Ben Saanane msahuri wa mweneyekiti wa CHADEMA

Sakata la kutoweka kwa afisa wa cheo cha juu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Ben Saanane limechukua sura mpya baada ya chama hicho kutoa tamko rasmi kwamba hawajui alipo msaidizi huyo wa mwenyekiti wa taifa CHADEMA,

Kupitia mwanasheria mkuu wake Tundu Lissu, chama hicho kimeitaka serikali kupitia jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya mahali alipo Ben Saanane, msaidizi wa mwenyekiti wa taifa upande wa siasa na jamii, anayedaiwa kutoweka tangu Novemba 14 mwaka huu na mara ya mwisho kupata taarifa zake inadaiwa aliwasiliana na mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.

Tundu Lissu akizungumza na waandishi habari mjini Dar es Salaam
Tundu Lissu akizungumza na waandishi habari mjini Dar es Salaam

Tundu Lissu amesema serikali ndio yenye ulinzi na udhibiti mkubwa wa mipaka ya nchi ambapo inao uwezo wa kufahamu kama mtu ametoka nje ya nchi au yupo ndani ya nchi hivyo wanawajibu wa kufanya kila njia ya kumpata Ben Saanane ambaye taarifa za kutoweka kwake kwa mara ya kwanza zilitolewa na ndugu zake wa karibu.

“Wakisema wamemkamata tutawauliza kwa nini wamemkamata na kumshikilia muda wote. Hatumtuhumu mtu yoyote tutauliza masuala ambayo yanahitaji kuulizwa. Huyu Ben Saanane kuna kipindi aliandikiwa barua ya kutishwa,” alisema Lissu.

Katika hatua nyingine CHADEMA pia imetaka uchunguzi wa kutosha juu ya maiti za watu zilizookotwa mto Ruvu ili kujiridhisha aina ya kifo chao licha ya kwamba taarifa za awali zilidai watu hao ni wahamiaji haramu.

Lissu alisema,” Serikali kwa maana ya jeshi la Polisi wanatakiwa kufanya inquest. Inquest ni uchunguzi wa sababu za kifo. Ilikujibu suali hiki kifo kimesababishwa na jinai au ni kifo cha kawaida."

Akanongezea kufafanua kwamba,” wale wataalamu wa uchunguzi (pathologists) lazima wafanye uchunguzi wakitaalamu kutambua huyu mtu amekufa kwa sababu gani.”

Hata hivyo Mwandishi wa VOA Dina Chahali anasema maiti za watu saba wasiojulikana ziliokotwa katika mto Ruvu mkoani pwani Desemba 11 mwaka huu.

Taarifa za awali kutoka polisi zilieleza kwamba miili hiyo inasemekana ni ya wahamiaji haramu, na tayari imezikwa. waziri mkuu Kassim Majali katika maadhimisho ya Maulid hivi karibuni pia aliagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi wa vifo hivyo na kutoa taarifa kamili.

XS
SM
MD
LG