Chama kikuu cha upinzani nchini Uganda-FDC kimeitisha maandamano makubwa ya wafuasi wake yanayolenga kuilazimu serikali kuitikia ukaguzi wa lazima wa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Februari mwaka huu.
FDC iliiandikia polisi maombi ya kutaka kuruhusiwa kuandamana inavyohitajika kisheria huku chama hicho kikitaka ulinzi wa polisi wakati wa mandamano hayo na kuonya kwamba iwapo polisi watawanyima kibali chama hicho kilisema itabidi kutumia nguvu.