Uganda bado iko katika hali ya shauku kubwa huku watu wakisubiri matokeo ya uchaguzi baada ya kupiga kura siku ya Alhamisi.
Rais Yoweri Museveni aliyoko madarakani kwa miaka 30 anapata changamoto kutoka kwa wagombea saba wa upinzani.
VOA ilikuwa mitaani kufuatilia uchaguzi huo kama anavyoeleza mwandishi wetu Sunday Shomari jinsi uchaguzi ulivyoanza.
Sasa watu kila pembe ya dunia wanasubiri kusikia nani aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo.