Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 10:36

Besigye ajibu kauli ya Museveni


Mgombea wa urais katika uchaguzi wa Febuari 18 nchini Uganda, Dkt Kiiza Besigye amejibu kauli iliyozua utata iliyotolewa na Rais wa Uganda Yoweri Museveni.
Siku chache zilizopita Rais Yoweri Museveni alitamka kwamba Uganda ni shamba lake la ndizi na hawezi kuondoka wakati ndizi zinakaribia kukomaa.
Museveni aliongeza kusema kwamba hawezi kumruhusu mtu yeyote kuzivuna ndizi za shambani kwake.
Kufuatia matamshi hayo kiongozi wa chama cha FDC, Dkt Kiiza Besigye, yeye amemlinganisha Rais Museveni na mti mkubwa uliotikiswa sana, mizizi yake kukatika na unaokaribua kuanguka wakati wowote.
Usemi wake Besigye umekaribiana na mgombea mwengine wa urais Amama Mbabazi, ambaye alikuwa mjini Busia, Jumatano na kuwataka wapiga kura katika eneo hilo kumuondoa Museveni madarakani ili kujiendeleza kiuchumi.
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:56 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

XS
SM
MD
LG