Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 08:14

Msemaji wa Putin asema, rais huyo ni mzima


Rais wa Russia, Vladimir Putin
Rais wa Russia, Vladimir Putin

Msemaji wa rais wa Russia, Vldimiri Putin, amekana tetesi zilizopo kwamba kiongozi huyo wa taifa ana matatizo ya afya.

Dmitry Peskov, amekiambia kituo kimoja cha redio nchini Russia, kwamba rais huyo mwenye umri wa miaka 62 ni mwenye afya njema.

Ufafanuzi huo unatolewa kufuatia uvumi ulio zagaa kwenye tovuti za lugha ya Kirusi na mitandao ya kijamii zinazoeleza bwana Putin, anaumwa ama amekufa, ameondolewa madarakani ama yuko katika mvutano mkali kati ya makundi yanayopingana ndani ya chama tawala cha nchi hiyo.

Rais huyo wa Russia, hajaonekana hadharani toka alipokutana na waziri mkuu wa Italia, Matteo Renzi mjini Moscow Machi 5.

Mkutano wake na marais wa Kazakhstan, na Belarus, Alhamisi na Ijumaa umeahirishwa na sababu zilizotolewa ni kwamba Putin, ni mgonjwa.

XS
SM
MD
LG