Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 13:43

Chad na Niger yafanyashambulia Boko Haram


Mjeshi ya Chad, na Niger, yameanzisha mashambulizi ya pamoja dhidi ya kundi la kiislamu la Nigeria Boko Haram.

Vyanzo vya jeshi vinasema vikosi vya nchi hizo mbili vilianza mashambulizi yao Jumapili, kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno.

Mataifa hayo mawili yanajiunga na Cameroon, na Nigeria, katika mapambano dhidi ya kundi hilo ambalo hivi karibuni limejionyesha kulifuata kundi la Islamic State.

Siku ya jumamosi kundi la uangalizi wa makundi ya Jihad SITE lilinukuu Boko Haram, ikisema inatangaza kutii himaya za kiislamu katika mkanda wa video.

Mkanda huo wa video unaosadikika kuwa kundi la kigaidi la Nigeria, la Boko Haram.

XS
SM
MD
LG