Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 10:31

AU yataka jeshi la Burkina faso kukabidihi madaraka kwa raia.


Luteni Kanali Isaac Zida, kiongozi wa muda wa Burkina Faso akisalimiana na mabalozi, Nov. 3, 2014 huko Ouagadougou.
Luteni Kanali Isaac Zida, kiongozi wa muda wa Burkina Faso akisalimiana na mabalozi, Nov. 3, 2014 huko Ouagadougou.

Umoja wa Afrika umeipa jeshi la Burkina Faso muda wa wiki mbili kurudisha madaraka kwa serikali ya mpito ya kiraia.

Baraza la usalama na Amani la Umoja wa Afrika lilieleza jana kwamba halitaiwekea vikwazo Burkina Faso kwa sasa lakini imesema jeshi lazima likibadhi madaraka kwa serikali ya kiraia au la sivyo kukiona.

Rais wa muda mrefu wa Burkina Faso Blaise Compaore alijiuzulu Ijumaa baada ya maandamano ya ghasia kupinga juhudi zake za kujaribu kuongeza muda wa utawala wake uliodumu kwa miaka 27 kwa kubadili katiba.

Jeshi lilichukua udhibiti wa nchi na kumteuwa Luteni kanali Isaac Zida kama rais wa muda. Vyombo vya habari vinamnukuu kwamba atakabidhi madaraka kwa baraza la mpito litakaloongozwa na kiongozi atakayeteuliwa kwa maridhiano, lakini hakusema lini hilo litafanyika.

XS
SM
MD
LG