Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 12:29

Marekani yashikwa na hofu ya Ebola


Gari la kubeba wagonjwa likiwa limembeba Nancy Writebol aliyeathiriwa na ugonjwa wa Ebola.
Gari la kubeba wagonjwa likiwa limembeba Nancy Writebol aliyeathiriwa na ugonjwa wa Ebola.

Uongozi wa rais Barack Obama wa Marekani umetoa wito wa kuwepo hali ya utulivu kufuatia kupatikana kwa mgonjwa wa ebola nchini kwake.

Taarifa zinasema Marekani inajiandaa kupambana na mzozo wa ugonjwa wa ebola kote nchini mwake na katika eneo.

Milipuko wa ugonjwa wa ebola kwa miaka 40 iliyopita ilidhibitiwa. Marekani inatuma vikosi elfu mbili nchini Liberia kusaidia kupambana na mlipuko wa ebola ambao umeuwa takriban watu elfu tatu katika bara la Afrika magharibi.

Marekani pia inajaribu kuondoa hofu kuhusu kuzuka kwa ugonjwa wa ebola nchini mwake.

Raia wa Liberia Thomas Duncan yuko katika hali mbaya lakini inayoweza kudhibitiwa katika hospitali moja kwenye jimbo la Texas baada ya kuambukizwa virusi vya ebola kabla ya kuondoka Liberia kuingia marekani.

XS
SM
MD
LG