Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 20:17

Majeshi ya Somalia, AU wakomboa miji kadhaa kutoka kundi la Alshabab.


Mwanajeshi wa Umoja wa Afrika katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu ambao sasa unadhibitiwa na serikali na kulindwa na majeshi ya AU. August 12, 2011
Mwanajeshi wa Umoja wa Afrika katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu ambao sasa unadhibitiwa na serikali na kulindwa na majeshi ya AU. August 12, 2011
Majeshi ya Somalia na yale ya Umoja wa Afrika (AU) wamekomboa miji kadhaa kutoka kwa wanamgambo wa Al-shabab katika kile walichokiita juhudi mpya za kuliondoa kundi hilo kutoka kwenye ngome zake nchini humo.

Moja ya maeneo ni katika mji wa Burdhubo ambao ulikuwa ni ngome kuu ya Alshabab kusini mwa Somalia. Majeshi kutoka Umoja wa Afrika nchini Somalia yajulikanayo kama AMISOM na jeshi la taifa la Somalia yalichukua tena udhibiti wa eneo hilo Jumapili baada ya siku moja ya mapigano.

Kanali Ali Hamud msemaji wa AMISOM aliimbia VOA kwamba wapiganaji wa Alshabab wanarudi nyuma mara tu wanapoona majeshi ya AMISOM, lakini hilo bado linaangaliwa ikiwa badala yake wanajipanga kwa vita vya msituni.

Miji mingine ambayo jeshi la Somalia na AMISOM wamekomboa tangu Ijumaa ni pamoja na Weel Dehyn,Wajid,Rabdhure Ted na Hudur. Wako katika mikoa ya Gedo na Bakool karibu na mpaka wa Ethiopia na kilometa chache kutoka mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
XS
SM
MD
LG