Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 18:22

Mpelelezi wa ki-Palestina asema Israel ndio mshukiwa mkuu wa kifo cha Arafat.


Kiongozi wa zamani wa Palestina hayati Yasser Arafat.
Kiongozi wa zamani wa Palestina hayati Yasser Arafat.
Mpelelezi wa ki-Palestina anasema Israel ndio mshukiwa wa kwanza mkuu na pekee wa kifo cha rais Yasser Arrafat, baada ya wanasayansi wa Uswiss kusema kuwa kulikuwa na ushahidi wa kiasi kuwa alipewa sumu yenye mnunurisho.

Tawfik Tirawi mpelelezi mkuu wa ki-Palestina anayechunguza kifo cha Arafat aliwaambia waandishi wa habari Ijumaa huko Ramaallah kwamba uchunguzi utaendelea alikielezea kifo cha Arafat kuwa ni uhalifu wa karne ya 21.

Maelezo hayo yametolewa baada ya wanasayansi wa ushahidi wa Uswiss kusema kuwa wamepata ushahidi wa kiwango fulani unaounga mkono wazo kwamba kiongozi huyo wa Palestina alipewa sumu inayosababisha kifo ya mnunurisho wa Polonium.
XS
SM
MD
LG