Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:29

Obama aunga mkono diplomasia Syria lakini shambulizi la kijeshi bado lawezekana.


Obama akilihutubia taifa kwa njia ya televisheni kuhusu maamuzi yake huko Syria.
Obama akilihutubia taifa kwa njia ya televisheni kuhusu maamuzi yake huko Syria.
Rais Obama ameeleza mpango wake wa kuzuia serikali ya Syria kutumia silaha za kemikali jumanne na rais aliunga mkono kwa tahadhari pendekezo la Russia kutanzua mzozo huo.

Obama amesema shambulizi la Marekani huko Syria litakuwa lenye malengo maalum katika kuharibu matumizi ya kemikali.

Rais amesema hatapeleka wanajeshi wa Marekani huko Syria na hatafanya operesheni isiyojulikana mwisho wake kama vile Iraq na Afghanistan na mashambulizi ya ndege ya muda mrefu kama ilivyokuwa Libya au Kossovo.

Amesema anajua hali mbaya ya vifo viliyosababishwa na vita vya Iraq na Afghanistan , kwamba wazo lolote la vita halitapendwa na watu.
XS
SM
MD
LG