Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 18:58

M23 wataka mazungumzo baada ya kushindwa Goma.


Jeshi la Congo FADRC baada ya kusambaratisha vikosi vya M23 huko Kibati..
Jeshi la Congo FADRC baada ya kusambaratisha vikosi vya M23 huko Kibati..
Kundi la M23 la jamhuri ya kidemokrasi ya kongo linasema linasitisha mapigano na jeshi la Congo na kuondoka kwenye eneo ambalo mapigano yalikuwa makali katika siku za karibuni ili kuruhusu uchunguzi huru ufanyikwe kuhusiana na mizinga iliyoshambulia Rwanda .

Rwanda jana imeituhumu majeshi ya serikali ya congo kwa kufyetua mizinga na roketi ndani ya ardhi yake , lakini umoja wa mataifa na serikali ya Kigali wanakilaumu kundi la M23 kwa mashambulio hayo.

Kiongozi wa kundi la M23 Bertrand Bisimwa aliiambia VOA kwamba wapiganaji wake wanaondoka kwenye maeneo yao katika kijiji cha Kanyaruchinya , karibu na Goma kwenye mpaka wa Congo na Rwanda ili kuruhusu uchunguzi ufanyike kuamua nani hasa alihusika.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:28 0:00
Kiungo cha moja kwa moja


Naye msemaji wa majeshi ya serikali FARDC Olivia Amuli akizungumza na VOA amesema kwamba wanajeshi wa serikali wamerudisha nyuma wapiganaji wa M23 jana na M23 wameondoka kwasababu ya kupata pigo kubwa aliongeza kuwa baada ya mapambano ya siku 9 hatimaye wamedhibiti maeneo ya Kibati na Kilimanyoka na kusema waasi hao wamekimbia huku wakiwa wameacha magari yao yaliopigwa na mabomu.

Wakati huo huo msemaji wa jeshi la Congo alishiriki kwenye mjadala na idhaa ya Kiswahili ya VOA msemaji huyo wa serikali alieleza kwamba M23 wamepiga mabomu huko Goma na nchini Rwanda ili wapate usaidizi wa Rwanda huko Congo na sasa wameondolewa huko Kibati akidai kuwa M23 wanadanganya wananchi . Kusikiliza mahojiano hayo bofya hapa.
please wait

No media source currently available

0:00 0:17:03 0:00
Kiungo cha moja kwa moja
XS
SM
MD
LG