Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 16:35

Maandamano yazuka baada ya Zimmerman kuachiwa huru


Maandamano baada ya George Zimmerman kuachiwa huru,Times Square, New York, Julai 14, 2013.
Maandamano baada ya George Zimmerman kuachiwa huru,Times Square, New York, Julai 14, 2013.
Rais wa Marekani Barack Obama ameomba kuwe na hali ya utulivu Jumapili baada ya mahakama moja katika jimbo la Florida kuamua kuwa George Zimmerman aliyekuwa akifanya doria za kujitolea katika mtaa wake hana hatia.

Uamuzi huu ulifuatia kesi iliyofuatiliwa kwa karibu na umma wa Marekani ambapo Zimmerman alishtakiwa kwa kumpiga risasi na kumuua kijana M’marekani mweusi asiyekuwa na silaha.

Katika taarifa ya maandishi bw.Obama alisema mauaji ya Trayvon Martin yanahuzunisha familia yake na Wamarekani.Kesi hiyo pia imetawala vyombo vya habari vya Marekani kwa wiki kadha sasa. Kulizuka maandamano ya amani katika miji kadhaa ya Marekani kufuatia uamuzi huo, wengi wakisema ‘ikiwa hakuna haki hakutakuwa na amani’

Rais Obama aliomba kuwe na utulivu akisema Marekani ni taifa linalofuata sheria na kwamba baraza la mahakama limeamua.

Kesi dhidi ya Zimmerman iliamuliwa Jumamosi usiku. Baraza la majaji likisema limefikia maamuzi ya kauli moja kwamba hana hatia. Uamuzi huo ulitangazwa moja kwa moja kwenye televisheni za Marekani na mitandao ya mawasiliano ya Internet na kuzua mjadala wa kitaifa kuhusu ubaguzi wa rangi na kesi za uhalifu nchini Marekani.

Martin mwenye umri wa miaka 17 aliuwawa mwaka jana katika makabiliano na Zimmerman aliyekuwa na bunduki. Zimmerman ni mwana wa M’marekani mzungu na mama mwenye asili ya kihispania.
XS
SM
MD
LG