Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 12:23

Hali ya utulivu yarejea huko Eritrea.


A U.N. peacekeeper stands guard at the U.N. Mission in South Sudan (UNMISS) base in Malakal, where some 19,000 people have been sheltering for nearly half a year.
A U.N. peacekeeper stands guard at the U.N. Mission in South Sudan (UNMISS) base in Malakal, where some 19,000 people have been sheltering for nearly half a year.
Hali ya utulivu yaripotiwa kurejea tena huko Eritrea siku moja baada ya kundi la askari waasi kujaribu kuchukua wizara ya mambo ya habari ya nchi hiyo.
Zaidi ya askari waasi 100 walivamia wizara hiyo huko Asmara mapema Jumatatu na kuwaamrisha watangazaji wa habari wa Televisheni ya kitaifa kusoma taarifa ya kudai kuachiwa kwa wafungwa wa kisiasa na kusema katiba ya 1997 itaheshimiwa.
Haikujulikana mara moja jinsi gani hali hiyo ilivyotulizwa lakini wanajeshi hao inaaminika waliondoka wizarani hapo Jumatatu usiku.
Katika ujumbe uliotolewa kwenye mtandao wa Twitter Jumanne mkurugenzi wa ofisi ya rais wa Eritrea Yemane Ghebremeskel amesema hali sasa ni tulivu.
XS
SM
MD
LG