Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 17:19

Wamarekani kuhitimisha upigaji kura Jumanne.



Jumanne ni siku muhimu kwa wapiga kura wa Marekani kuhitimisha zoezi la upigaji kura katika majimbo yote ili kumpata mshindi katika uchaguzi wa urais ulio na ushindani mkubwa.

Rais wa Marekani Barack Obama na mpinzani wake Mitt Romney siku ya jumatatu walifanya kampeni za dakika za mwisho kwa wapiga kura katika majimbo muhimu ikiwa imebakia siku moja kabla ya uchaguzi katika juhudi za mwisho kuvunja ushindani.

Katika majimbo ya wisconsin , rais Obama alimshutumu bwana Romney kwa kujaribu kurejesha mawazo mabaya aliyoyatoa kabla na kusema taifa haliwezi kufanikiwa bila kuwa na daraja la kati lenye nguvu.

Kwenye mkutano wa jana asubuhi katika jimbo la kusini la Florida bwana Romney aliwaambia wafuasi wake kwamba kiongozi huyo aliyoko madarakani Mdemocrat ameshindwa kutekeleza ahadi zake wakati aliposhinda kiti cha urais mwaka 2008.
XS
SM
MD
LG